Breaking News
recent

WANAJESHI WA NCHI YA KENYA WAUAWA NA KUNDI LA AL SHABAB......


Wapiganaji wa Al Shabaab
Serikali ya Kenya imethibitisha kuwa maafisa wake wawili wa jeshi wameuawa na wengine wawili kujeruhiwa, baada ya wapiganaji wa Kiislamu wa Al Shaabab kufanya shambulio la kuvizia, baada magari yao kukwama barabarani huko Somalia.
Ripoti zinasema msafara wa wanajeshi wa Kenya ulikuwa ukielekea eneo la Ras Kamboni wakati shambulio hilo lilipotokea.
Kamanda wa polisi mjini Mombasa Robert Kitur amethibitishia bonifacemjailablog kuwa shambulio hilo limetokea.
Kwa upande wao, msemaji wa Al shabaab, Abu Mus'ab amedai kuwa wapiganaji wake walifanikiwa kuteketeza magari kadhaa ya jeshi la Kenya, madai ambayo yamekanushwa vikali na utawala nchini kenya.
Aidha amesema wa wapiganaji kadhaa wa Al shabaab waliuawa na wengine kujeruhiwa wakati wa makabiliano hayo.

Unknown

Unknown

No comments:

Powered by Blogger.