Breaking News
recent

SPIKA WA BUNGE APATIKANA HAI KENYA


Spika wa bunge la Embu nchini Kenya amepatikna baada ya kutekwa nyara yapata siku nne zilizopita.
Bwana Justus Kariuki Mate alipatikana hoi na wafanyi biashara wa kuuza mboga katika eneo lenye baridi kali la Limuru viungani mwa mji mkuu wa Nairobi.

Spika huyo amekuwa mstaari wa mbele kuongoza juhudi za kumng'oa mamlakani gavana wa jimbo la Embu Martin Wambora.
Wafuasi wake wakiongozwa na naibu wake Ibrahim Swaleh pamoja na seneta wa jimbo hilo Lenny Kivuti walimtembelea hospitalini ambako amelazwa ilikupata matibabu.
Spika huyo aliwaambia wafuasi wake 
kuwa ndio kwanza mkoko umealika maua Embu kwani ataendelea na juhudi za kupalia na kukuza demokrasia.
Spika huyo anakabiliwa na madai kuwa alipuuza maagizo ya mahakama ya kusitisha mswada wa kumng'oa Mamlakani gavana wa Embu kwa kukiuka maadili ya ununuzi wa bidhaa na huduma za umma nchini kenya.
Spika huyo aliruhusu mjadala huo kuendelea mbele licha ya makataa ya korti.
Afisa mmoja wa kitengo cha jinai Nicholas Muriuki Kangangi alifikishwa mahakamani kwa dai ndiye aliyemteka nyara Spika huyo wa Bunge alipokuwa katika mkutano na washika dau mjini Nairobi.
Polisi wamesema wanaendelea kuchunguza tukio hilo linalotishia kuenea kwa demokrasia nchini Kenya.
Unknown

Unknown

No comments:

Powered by Blogger.