Breaking News
recent

MWANASHERIA MKUU WA ZANZIBAR AFUKUZWA KAZI ... SOMA ZAIDI

(Aliyevaa suti ya kijivu ni Mwanasheria wa Zanzibar aliyefutwa kazi)

Raisi wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein ametumia kipengele cha sheria kinachomruhusu kumbadilisha Mwanasheria Mkuu na kumfuta kazi mwanasheria mkuu wa Zanzibar  Othman Masoud Othman.

Katika habari iliyotolewa muda mchache uliopita na Televisheni ya ITV ilisema nafasi ya mwanasheria huyo imechukuliwa na aliyekuwa msaidizi wake katika nasfasi hiyo Said Hassan Said.

Kabla ya kufukuzwa kazi mwanasheria huyo alitolewa katika Bunge la Katibauma lililopita kutokana na kitendo chake cha kukosoa rasimu ya tatu ya katiba, kitendo ambacho kilizua tafrani bungeni huku wabunge wengine wakimuita masaliti.

                                                                               SOURCE: ITV

Unknown

Unknown

No comments:

Powered by Blogger.